• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

Kansa ya Mlango kizazi tishio kwa wanawake.

Posted on: April 27th, 2018

Saratani  ya mlango  wa kizazi ni ugonjwa ambao umekuwa ukisababisha mateso na vifo vingi kwa wanawake.

Hayo  yamesemwa  leo  tarehe 27/04/2018 na Mkuu wa  wilaya  ya Longido Mh. Daniel G. Chongolo wakati  wa uzinduzi wa chanjo ya kuzuia  saratani ya mlango wa kizazi kwa watoto wenye umri wa miaka 14 na maadhimisho ya wiki ya  chanjo  kiwilaya  yaliyofanyika  Katika kituo  cha Afya Longido.

Mh. Chongolo  amewaasa wasichana   kuacha kujamiiana katika umri mdogo kwani hiyo imekuwa ni moja ya sababu inayochangia  saratani  ya mlango wa kizazi.

Aidha Mh. Chongolo  amewataka  wazazi na walezi  kuhakikisha  wasichana  wote waliofikia umri  wa miaka 14 wanapatiwa chanjo  hiyo ili kuwaepusha na hatari ya kuja kuathiriwa na ugonjwa huo.


Kwa upande wake Kaimu  Mkurugenzi Mtendaji  ambaye pia ni Afisa Elimu Wilaya Ndg. Gerson Mtera amewataka wasichana hao kuwa  wajasiri ili waweze kupata chanjo hiyo na kuwakinga  na madhara  makubwa yanayoweza  kuwapata.


Akitoa maelezo ya chanjo hiyo Mratibu wa huduma ya mama na mtoto Wilaya Ndg. Josiah Mruve amesema walengwa wa chanjo  Kwa mwaka huu wa 2018  ni wasichana wote  waliotimiza  miaka 14, na kwamba kwa wilaya ya Longido matarajio ni kuchanja  wasichana 2,271 kulingana na sensa iliyofanyika Katika shule  zote na katika jamii.


Kwa upande wake mwanafunzi Sara Joel  Laizer amabye amekuwa wa kwanza kupatiwa chanjo hiyo katika wilaya ya Longido ameishukuru serikali kwa kuwajali watoto wa kike na kuona umuhimu wa kutoa chanjo hiyo ili kuwakinga na athari ya saratani hiyo ya mlango wa kizazi.

Amesema wanawake  wengi  wanakufa  Kwa ugonjwa huu  wa Kansa ya mlango  wa  kizazi jambo ambalo lingeachwa liendelee lingekuwa na madhara makubwa kwa jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.