• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

DC NG'UMBI AKABIDHI MRADI WA MBUZI 164 KWA KAYA MASKINI

Posted on: April 20th, 2023

Walengwa 43 wa kaya maskini katika kijiji cha Orbomba leo tarehe 20/04/2023 wamepewa mbuzi takribani 164  aina ya ISIOLO na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya jamii (TASAF),makabidhiano hayo yamefanyika katika ofisi ya kijiji cha Orbomba.

Akikabidhi mradi huo wa mbuzi aina hiyo ya ISIOLO kwa walengwa 43, Mheshimiwa Marko Ng'umbi mkuu wa Wilaya ya Longido amewataka wanakaya kuwatunza mbuzi hao kwa lengo la kuondoa umaskini kwenye kaya. Mbuzi hao wakiwatunzwa vizuri  watawasaidia kuongeza kipato kwani tunafahamu kuna faida nyingi sana kwenye mifugo hii ya mbuzi ikiwepo nyama, Maziwa, na wanapozaliana tutapata mbuzi wengi hapo sasa ndipo mnaweza kuwauza nakujipatia pesa kwa ajili ya chakula, mavazi, makazi bora pamoja na kusaidia kuwapeleka watoto shuleni.

Pamoja na hayo Mheshimiwa mkuu wa wilaya amewaasa wanakaya kutowapeleka sokoni mifugo hiyo hivi karibuni badala yake wawatuze mpaka watakapozaliana ndipo wanaweza kuwapeleka sokoni mana watakuwa wengi,kwa kuwa mradi umelenga kuongeza kipato kwa kaya hizo maskini. sambamba na hilo amewaomba wahakikishe mifugo hiyo inakuwa salama, "Ndugu zangu sitopenda kusikia mbuzi hawa tuliowagawia leo wanakufa au wamepotea ama wamepata madhara yeyote yale  badala yake nitafurahi nikisikia wako vizuri wana afya njema na wameongezeka kwa maana wamezaliana ili tujikwamie kiuchumi, badala ya kula mlo mmoja ama kushinda njaa na kulala njaa kabisa sasa tukiweza kuwatunza tutakula milo mitatu bila shida wala tatizo lolote "Alisema Mheshimiwa Ng'umbi

Nae mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Longido ndugu Stephen Ulaya ameishukuru Serikali  kwa kuwezesha kufanikisha mradi huo kwa kaya Maskini unaotekelezwa na TASAF awamu ya III,vilevile amewasihi sana wanakaya kuwatunza mbuzi hao ili waweze kuwasaidia kiuchumi

Akizungumza kwa niaba ya wanakijiji na wanakaya hao wa kaya maskini mwenyekiti wa kijiji cha Orbomba ndugu Lashilo Alais Ameishukuru wadau wa Mfuko wa Maendeleo ya jamii TASAF pamoja na serikali ya awamu ya Sita chini ya uongozi wa mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wananchi wake na kuwapatia mbuzi hao kwa lengo la kujikwamua kiuchumi na ameahidi kuwatunza kwa kila hali ili waweze kuwaletea manufaa katika kuongeza uchumi wa kaya.

Pia ameongeza kwa kuiomba Serikali kuwakumbuka zaidi kwani bado kuna kaya nyingi zinahitaji msaada kama huu ili ziweze kujikwamua na wimbi hili la umaskini. "Tunaiomba Serikali iendelee kutufikiria kwani bado kuna wananchi wengu huku kwetu wanauhitaji, hawa ni wachache tu ila bado wako wengi kijijini maisha yao ni changamoto "Alisema ndugu Kashilo Alais.


*JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KAZI IENDELEE*

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.