• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

WANAFUNZI 5,188 KUFANYA UPIMAJI WA KITAIFA DARASA LA NNE LONGIDO

Posted on: October 21st, 2025

NA ABRAHAM NTAMBARA, LONGIDO

Jumla ya wanafunzi 5,188 wa Darasa la Nne wanatarajiwa kufanya Mtihani wa Upimaji wa Kitaifa katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido, mkoani Arusha kuanzia kesho Oktoba 22 hadi 23, 2025.

Akizungumza leo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Mkuu wa Idara ya Utawala na Utumishi, Bw. Peter Matemba, amesema maandalizi yote muhimu yamekamilika huku wanafunzi wakiwa tayari kwa mtihani huo muhimu katika safari yao ya kielimu.

“Kama wilaya tumejipanga vizuri, wanafunzi wameandaliwa vya kutosha. Tunawaomba wazazi wawaandae watoto wao vizuri na kuhakikisha wanafika shuleni mapema kwa ajili ya kufanya mtihani. Vilevile, tunatoa wito kwa wanafunzi wenyewe kujiandaa kwa bidii,” alisema Bw. Matemba.

Kati ya watahiniwa hao, wavulana ni 2,726 na wasichana 2,462. Mtihani huo utafanyika katika shule 70, zikiwemo shule 57 za serikali na 13 zinazomilikiwa na mashirika ya dini pamoja na shule binafsi.

Bw. Matemba aliongeza kuwa walimu wakuu wameelekezwa kuandaa mazingira rafiki kwa ajili ya mtihani huo na kwamba semina mbalimbali zimefanyika kwa ajili ya kuwaandaa wasimamizi wa mitihani kuhakikisha uendeshaji wake unafanyika kwa ufanisi.

"Maandalizi yote muhimu tumeyakamilisha. Tunawatakia heri na baraka wanafunzi wetu wote katika upimaji huu wa kitaifa," aliongeza.

Kwa upande wake, Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Longido, Mwalimu Donat Bunonus, alisema wanafunzi wamepewa maandalizi ya kutosha na ana imani kuwa watafanya vizuri. 

“Naomba wazazi wawaruhusu watoto wao kufika shuleni kwa wakati, na kwa wanafunzi nawahimiza wajibu mitihani yao kwa kuzingatia yale waliyojifunza kutoka kwa walimu wao,” alisema Mwalimu Bunonus.

Mtihani huu wa Upimaji wa Kitaifa ni kipimo muhimu cha kutathmini uwezo wa wanafunzi na kuandaa msingi bora kwa maendeleo yao ya kitaaluma.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • WANAFUNZI 5,188 KUFANYA UPIMAJI WA KITAIFA DARASA LA NNE LONGIDO

    October 21, 2025
  • WWF YADHAMIRIA KUREJESHA MAZINGIRA ASILIA YA LONGIDO

    October 20, 2025
  • MATUKIO KATIKA PICHA SIKU YA PILI YA MAFUNZO YA WWF KWA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU UHIFADHI WA MAZINGIRA LONGIDO

    October 16, 2025
  • WWF YAWANOA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU SERA YA UTUNZAJI MAZINGIRA LONGIDO

    October 15, 2025
  • View All

Video

KARIBU LONGIDO LANGO LA UTALII
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.