• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

VIONGOZI WA DINI WILAYA YA LONGIDO WATOA TAMKO JUU YA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

Posted on: October 23rd, 2025

Na Mwandishi Wetu, LONGIDO

VIONGOZI wa dini wilayani Longido wamewataka wananchi kuendelea kudumisha amani na kupuuza taarifa za uvumi kuhusu maandamano, wakisisitiza umuhimu wa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Tamko hilo limetolewa leo na Kamati ya Haki na Amani ya Wilaya ya Longido katika kikao kifupi cha majadiliano kilichofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya, kikihusisha viongozi wa dini zote kwa lengo la kuhimiza mshikamano na utulivu kuelekea uchaguzi huo.

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wa dini, Sheikh wa Wilaya ya Longido, Sheikh Ramadhani Mpangala, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, alisema wananchi wanapaswa kuepuka kushiriki katika vitendo vya uvunjifu wa amani na badala yake kutumia fursa ya uchaguzi kuchagua viongozi wanaowataka kwa uhuru na utulivu.

“Tunaomba waumini na wananchi wote muendelee kudumisha amani. Msisikilize taarifa za uvumi kuhusu maandamano. Badala yake, mjitokeze kwa wingi siku ya Oktoba 29 kupiga kura kuchagua viongozi mnaowataka,” alisema Sheikh Mpangala.

Aidha, aliwaonya wananchi watakaojaribu kushiriki katika vitendo vya vurugu au uchochezi kuwa watachukuliwa hatua kali za kisheria na mamlaka husika, akisisitiza kuwa amani ya nchi ni jambo lisilopaswa kuchezewa.

Kwa upande wake, Katibu wa Kamati ya Haki na Amani, ambaye pia ni Mchungaji wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Simon Ole Morris, alisema amani ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa lolote, hivyo maandamano yasiyo na tija yanaweza kuvuruga utulivu na ustawi wa jamii.

“Watu wanaopanga kufanya maandamano wana nia ya kurudisha nyuma maendeleo ya taifa letu. Hakuna sababu yoyote ya kuandamana. Badala yake, watu wote waandamane kwenda kupiga kura,” alisema Mchungaji Morris.

Naye Katekista Aidan Couman kutoka Kanisa Katoliki, ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo, alisema kwa mujibu wa maandiko matakatifu, Mungu anawaagiza waumini wote kuishi kwa amani na watu wote, hivyo kushiriki katika vitendo vya uvunjifu wa amani ni kwenda kinyume na mapenzi ya Mungu.

Viongozi wengine walioshiriki kikao hicho ni pamoja na Mchungaji Elikana Paresso wa Kanisa la Anglikana na Mchungaji wa Kanisa Halisi la Mungu Baba Amani Halisi, ambao kwa pamoja waliwasisitizia wananchi, viongozi wa dini na serikali kushirikiana kulinda amani na utulivu wa taifa kabla, wakati na baada ya uchaguzi.

Mchungaji Amani Halisi alihitimisha kwa kuwataka wananchi wote wenye sifa ya kupiga kura kutumia haki yao ya kikatiba Oktoba 29, 2025, kuchagua viongozi watakaoliwakilisha kwa kipindi kijacho cha miaka mitano, akisema “kura ni silaha ya amani.


Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • VIONGOZI WA DINI WILAYA YA LONGIDO WATOA TAMKO JUU YA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 23, 2025
  • WANAFUNZI 5,188 KUFANYA UPIMAJI WA KITAIFA DARASA LA NNE LONGIDO

    October 21, 2025
  • WWF YADHAMIRIA KUREJESHA MAZINGIRA ASILIA YA LONGIDO

    October 20, 2025
  • MATUKIO KATIKA PICHA SIKU YA PILI YA MAFUNZO YA WWF KWA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU UHIFADHI WA MAZINGIRA LONGIDO

    October 16, 2025
  • View All

Video

KARIBU LONGIDO LANGO LA UTALII
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.