• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA MKOA WA ARUSHA MHESHIMIWA JOHN MONGELLA AMEFANYA ZIARA KWENYE MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI LONGIDO

Posted on: November 7th, 2023

 wa Mkoa wa Arusha pamoja na viongozi wa Mkoa leo tarehe 7/08/2023 ameanza ziara yake kutembelea na kujionea  miradi mbalimbali ya maendelaeo iinayotekelezwa  Wilayani humo.

Akizungumza na na viongozi wa wilaya ya Longido pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya mheshimiwa mkuu wa mkoa amewapongeza viongozi hao kwa kusimamia vema utekelezwaji wa shughuli za maendeleo "Kweli kabisa na kwa dhati niwapongeze sana viongozi wa Wilaya hii kwa kuwa mmeamka sasa kazi inaonekana Niwaombe tusimamie na tuongeze nguvu kwenye usimamizi wa miradi ili ikamilike kwa wakati, hakuna kipindi ambacho Serikali imetoa pesa nyingi kama wakati huu hivyo basi tumsaidie Mheshimiwa Rais kutekeleza ukamilishwaji wa miradi ndani ya wilaya"Alisema mheshimiwa Mongella.

Mheshimiwa mkuu wa mkoa amewaasa viongozi wasiogope kujifunza ili kufanya kazi iwe nyepesi, pia amewaomba kamati ya Siasa wilaya kuwa macho kwenye utekelezaji wa shughuli za maendeleo ili kutimiliza ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo imelenga kuleta Maendeleo kwa wananchi.

Mheshimiwa John Mongella na timu kutoka mkoani wametembelea miradi mbali mbali ikiwemo ujenzi unaoendelea wa shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mfano ya Mkoa mradi uliopokea fedha taklibani Shilingi Bilioni tatu (3)ambao ukamilishwaji wa shule hiyo ya mfano itachukua zaidi ya wanafunzi 800.

Pia ametembelea na kujionea ujenzi wa uzio wa shule ya Sekondari Longido pamoja na bweni la wavulana ujenzi unaoendelea shuleni hapo. 

Sambamba na hilo Mkuu Mkoa amepongeza kamati ya ujenzi kwa kushirikiana na kufanya kazi nzuri.

Pia Mheshimiwa  alitembelea baadhi ya majengo ya Hospital ya Wilaya ambako mbali na kupongeza pia ameagiza marekebisho madogo madogo yafanyike pamoja na kuweka umeme wenye nguvu kwenye  majengo yasio na umeme wenye nguvu ili wananchi waendelee kupatiwa huduma nzuri kwenye Hospital hiyo kwani vifaa vingi  vipo hivyo basi hakuna sababu ya kuendelea kuchelewesha baadhi ya huduma kwa watanzania

"Tafadhali naomba mjitahidi sana kukamilisha kwa haraka ujenzi wa bweni hili la wavulana ili wanafunzi hawa waweze kuingia na kuendelea na masomo yao bila matatizo yoyote, ofisi yangu ya mkoa itaunga mkono kwa kutoa bati 100 pamoja na mifuko ya sement  50 ofisi ya mkuu wa Wilaya itoe bati 50 na wazazi bati 100 sioni sababu ya ucheleweshaji wa ujenzi wa bweni hili "Alisema Mkuu wa Mkoa alupotembelea ujenzi wa bweni la wavulana shule ya Sekondari Ketumbeine unaojengwa kwa fedha za TASAF ambao serekali imetoa kiasi cha Shilingi Milion 155 na bweni hilo linataraji kuchukua zaidi ya wanafunzi 80.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Longido mheshimiwa Marco Henry Ng'umbi amemshukuru Mkuu wa Mkoa na wajumbe aliofuata nao kwa kutembelea na kujionea utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo Wilayani humo. Mkuu wa Wilaya ameishukuru sana Serikali ya awamu ya sita kwa kutoa pesa nyingi na kuwekeza kwenye miradi hii ya maendeleo Wilayani kwake, Mheshimiwa Ng'umbi ameahidi kuisimamia miradi yote kwa kushirikiana na viongozi wote waliopo Wilayani humo pamoja na wananchi ili waweze kujua nini serikali inafanya kwenye jamii yao"Mheshimiwa mkuu wa Mkoa sisi Longido tumejipanga vizuri sana kumsaidia Rais kwenye usimamizi na utekelezaji wa miradi kwenye Afya, Elimu maji na hata miundo mbinu ya barabara na Madaraja ". Alisema Mheshimiwa Ng'umbi

Nae Mzee Thobiko ambae ni mkazi wa kijiji cha Longido amemshukuru Mkuu wa Mkoa pamoja na wajumbe kwa kutembelea miradi ya maendelaeo," Tunamshukuru sana Rais Samia kwa kutupendelea Longido na kutupatia fedha nyingi , tunashukuru Mkuu wa Mkoa kwa kufika na kutembelea miradi tunayofuraha sana na tunamkaribisha sana Longido," Alisema mzee huyo.

Ziara ya mkuu wa Mkoa Wilayani Longido ni ya siku mbili ambapo tarehe 8/11/2023 Mheshimiwa atakamilisha ziara yake kwenye miradi ya maendeleo Wilayani humo.


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KAZI IENDELEE


Mheshimiwa Mongella alipo kuwa akikagua moja ya majengo ya Hospital ya Wilaya 

Mh. Mongella kwemye ujenzi wa bweni la wavulana Longido Sekondari. 



Mkuu

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • IDARA YA AFYA ,USTAWI WA JAMII NA LISHE YAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM