• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

MKUU WAILAYA YA LONGIDO MHE.SALUM KALLI AMESHIRIKI ZOEZI LA UGAWAJI WA DAWA ZA KINGA TIBA KATIKA KATA YA KIMOKOUWA WILAYANI LONGIDO.

Posted on: September 30th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mheshimiwa Salumu Kalli, leo tarehe 30 Septemba 2024, ameshiriki zoezi la ugawaji wa dawa za kingatiba dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza, kama vile trakoma na vikope, katika kata ya Kimokouwa, wilayani Longido. Halmashauri ya Wilaya ya Longido, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na wadau mbalimbali, imeendelea na mpango wa kupambana na magonjwa yasiyopewa kipaumbele kama vile minyoo ya tumbo, kichocho, vikope, usubi, na mabusha.

Magonjwa haya yamekuwa yakiathiri jamii, hasa zile zenye kipato cha chini na zinazokaa kwenye maeneo yenye upatikanaji mgumu wa huduma za afya. Mradi wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele umegawanyika katika sehemu mbili. Kwanza, utoaji wa dawa za minyoo na kichocho kwa watoto wenye umri wa miaka 5 hadi 14, na pili, utoaji wa dawa za vikope kwa watu wote isipokuwa watoto chini ya miezi sita, wajawazito, na wagonjwa mahututi.

Mratibu wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele wilayani Longido, Dk. Felix Mbise, akisoma taarifa ya umezeshwaji wa dawa za vikope, amesema kuwa mwaka 2022, zoezi la utoaji dawa kwa watoto lilifanikwa kwa asilimia 97.1, huku kwa watu wazima likifikia asilimia 88.6. Mwaka huu 2024, awamu ya kwanza imewafikia watoto 30,456 wenye umri wa miaka 5-14, huku watu wazima walengwa wakiwa ni 181,720. Awamu ya pili inatarajiwa kuwafikia walengwa 212,176, na zoezi la umezeshwaji wa dawa bado linaendelea kwenye kata zote wilayani Longido.

Akizungumza na wakazi wa kata ya Kimokouwa, Mheshimiwa Kalli amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi ili kumeza dawa hizo za kingatiba kwa manufaa ya afya zao na jamii kwa ujumla. "Niwaombe ndugu zangu tujitokeze kwa wingi kushiriki zoezi hili kwa ajili ya afya zetu. Bila kuwa na afya njema, huwezi kushiriki shughuli zozote za kimaendeleo, hivyo tuzilinde afya zetu," alisema Mheshimiwa Kalli.

Kwa upande wake, kiongozi wa kimila wa jamii ya Kimaasai, Laigwanani Ngulupa, ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwapatia dawa za kingatiba dhidi ya trakoma na vikope, magonjwa ambayo yamekuwa yakiwasumbua wafugaji, hususan katika maeneo yao ambako magonjwa haya huenea kupitia wadudu kama inzi. "Ninamshukuru sana Mkuu wa Wilaya ya Longido kwa kuja kwenye boma letu na kugawa kingatiba dhidi ya trakoma. Nawaomba wananchi wenzangu kujitokeza na kumeza dawa hizi kwa afya zetu," alisema Mzee Ngulupa.

Umezeshwaji wa dawa za Trakoma na vikopr ni zoezi endelevu kwa wananchi na wakazi wa Longido.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.