• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

SERIKALI YAAHIDI KUMALIZA KERO YA MAJI SHULE YA SEKONDARI NATRON FLAMINGO'S IFIKAPO JANUARI 2026

Posted on: October 14th, 2025

NA ABRAHAM NTAMBARA

SERIKALI ya Wilaya ya Longido imeahidi kuhakikisha changamoto ya upatikanaji wa maji ya uhakika katika Shule ya Sekondari Natron Flamingo's iliyopo Kijiji cha Meirugoi, Kata ya Gelai Meirugoi, wilayani humo, mkoani Arusha inakwisha ifikapo Januari 2026.

Ahadi hiyo imetolewa Oktoba 13, 2025 na Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Longido Mwl. Gilbert Sombe akizungumza katika Mahafali ya Saba (7) ya Kidato cha Nne ya Shule hiyo wakati akijibu Risala ya wahitimu, hotuba ya Mwalimu Mkuu sambamba na salamu za Mwenyekiti wa Kijiji cha Meirugoi ambao kwa pamoja walielezea juu ya changamoto hiyo na kumuomba aifikishe katika Vikao vya Halmashauri ili iweze kutatuliwa.

Hata hivyo Mwl. Sombe alikiri Serikali inafahama changamoto hiyo, na kusema kuwa Halmashauri kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Arusha (AUWSA) wanaendelea kuifanyia kazi na kwamba watahakikisha wanaimaliza haraka.

Kwamba wakati juhudi hizo zikifanyika, Mwl. Sombe aliiagiza Bodi ya Shule hiyo kuitisha vikao haraka iwezekanavyo ili kujadili namna gani wazazi wanaweza kushirikishwa katika kununua Matanki ya Maji ambayo yatatumika kuhifadhia maji ili yawe yanapatikana kwa muda mrefu.

"Kama Serikali tunatambua changamoto hii, hivyo tunaendelea kushirikiana na Mamlaka ya Maji kumaliza tatizo hili. Hata hivyo naomba Vikao vya Bodi vikae na kutoa maamuzi na sisi tutatekeleza," alisema Mwl. Sombe na kusisitiza,

"Nimatumaini yangu Mwenyekiti na Katibu wa Bodi mtakaa vikao haraka na kuangalia namna kila mzazi atachangia ununuzi wa Matanki. Naomba wazazi mshirikiane kununua Matanki ya Maji ili hata Maji yakiletwa yahifadhiwe, na sisi kama Serikali kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji tutahakikisha hadi kufikia Januari mwakani changamoto hii iwe imekwisha,".

Akizungumzia kuhusu Mahafali hayo ya Saba yaliyofanyika shuleni hapo ambayo yalikuwa na jumla ya wahitimu 126 kati ya Wanafunzi 167 walioanza Kidato cha Kwanza mwaka 2022, Mwl. Sombe alisema kutokana na historia ya Shule hiyo kuendelea kupanda kielimu, hategemei kuwepo Mwanafunzi hata mmoja atakayefeli mtihani.

Mwl. Sombe alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa wazazi kuwa karibu na watoto wao na kwamba wawe wanawatembelea Shuleni badala ya kwenda tu kipindi cha Mahafali, jambo ambalo litawafanya kujua changamoto zinazowakabili na kuweza kushirikia namna ya kuzitatua lengo likiwa ni kuwafanya watoto wasome katika mazingira mazuri.

Awali Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Hassan Hassan, alisema kuwa wamewaandaa vyema wahitimu hao na kuahidi kuwa watafauli vizuri mtihani wao na kwamba kama Walimu wamefanya sehemu yao na kuwataka wazazi kuendelea kuzungumza na vijana wao kuwaeleza umuhimu wa kusoma na nini jamii inategemea kutoka kwao.

"Vijana hawa tumewanyoosha vya kutosha, hivyo Wazazi sisi kama Walimu tumemaliza kwa nafasi yetu kuwafundisha, kwahiyo na ninyi ni zamu yenu kuwafundisha duniani kuna nini. Mshauri mtoto wako na umueleze nini maana ya kusoma na ajue jamii inategemea nini kutoka kwake," alisema Mwl. Hassan.


Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO September 04, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • WWF YAWANOA VIONGOZI WA DINI, VIJIJI NA VIONGOZI WA KIMILA KUHUSU SERA YA UTUNZAJI MAZINGIRA LONGIDO

    October 15, 2025
  • COMPASSION NA SERIKALI WAUNGANA KUMWEZESHA MTOTO WA KIKE NAMANGA

    October 13, 2025
  • SHULE YA SEKONDARI NATRON FLAMINGO'S YAUNGA MKONO MATUMIZI NISHATI SAFI YA KUPIKIA, YAFUNGA MFUMO WA GESI

    October 14, 2025
  • SERIKALI YAAHIDI KUMALIZA KERO YA MAJI SHULE YA SEKONDARI NATRON FLAMINGO'S IFIKAPO JANUARI 2026

    October 14, 2025
  • View All

Video

KARIBU LONGIDO LANGO LA UTALII
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.