• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST LONGIDO

Posted on: May 9th, 2023


Mkuu wa Wilaya ya Longido Mheshimiwa Marco Henry Ng'umbi amefungua rasmi kikao cha maelekezo ya utekelezaji wa mradi wa Boost unaofadhiliwa na Bank kuu ya Dunia leo tarehe 9 may 2023 katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Longido

Akitoa maelekezo hayo ya utekelezaji wa mradi huo wa Boost wa P4R (PAY FOR RESULTS) Mkuu wa wilaya amewataka wasimamizi wa mradi pamoja na walimu wa kuu walionufaika na mradi huo wa ujenzi wa shule za msingi pamoja na madarasa ya awali kuwa makini kwenye usimamizi wa mradi ili kupata majengo mazuri na viwango vya hali ya juu kwa kuwa mradi huu ni walipa kwa matokeo ili tuweze kupata fedha nyingine za kuendeleza mradi na miradi mingine mingi inayokusudiwa ndani na nje ya Halmashauri

"Sitegemei kuona tunashindwa kwenye kutekeleza mradi kwa namna yeyote ile maana hatuna sababu ya kushindwa"alisema Mheshimiwa Ng'umbi

Mheshimiwa Ng'umbi amewataka wasimamizi wa mradi huo kuwashirikisha kwa karibu wananchi ama jamii nufaika wa mradi ili kuwafanya wawe sehemu ya mradi kwani  wanaweza kusaidia kwenye shughuli za kawaida za utekelezaji kama kusogeza mawe kuchimba msingi, pamoja na shughuli nyingine ndogo ndogo

Pia amesisitiza sana kufuata taratibu zote za manunuzi, bidhaa zinunuliwe kihalali kwa utaratibu uliowekwa "Msithubutu kununua bidhaa kwa wazabuni mana hatutapata bidhaa bora na kwa bei nafuu" Alisema Mheshimiwa Ng'umbi

Sambamba na hilo ameomba mikataba ya mafundi kufuata taratibu na lazima ipitiwe na mwanasheria ili kudhibitisha ubora, ufanisi na uwezo wa kazi zake.

Naye mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Longido  ndugu Stephen A Ulaya ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa jitahada zake za kuboresha elimu katika shule  za msingi sambamba na ujenzi na uboreshwaji wa madarasa ya awali na ameahidi kusimamia mradi huo kwa karibu zaidi ili kurahisisha ufanisi wake.

"Mheshimiwa mkuu wa wilaya kwa niaba ya walimu wakuu wanufaika wa mradi tunaahidi kusimamia kazi hii kwa umakini na weledi wa hali ya juu ili tuweze  kupata miradi mingi na yenye tija kwa wanachi wetu"Alisema Mwalimu Deusdedit Afisa Elimu Msingi halmashauri ya wilaya ya Longido. 

*Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kazi iendelee*

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • DED LONGIDO AFUNGUA MAFUNZO UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

    May 14, 2025
  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM