• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YATOA TSHS. 4,200,000 KAMA KIFUTA MACHOZI/JASHO KWA WANANCHI LONGIDO

Posted on: May 13th, 2019

Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Ofisi ya Mkurugenzi Idara ya Wanyamapori imetoa malipo ya kifuta Machozi/Jasho cha Tsh. 4,200,000 kwa wakazi 13 wa Wilaya ya Longido waliojeruhiwa/kuumizwa na wengine kuuawa kwa kushambuliwa na wanyamapori hatari/wakali wakiwa katika shughuli zao za kila siku za hapa na pale mwaka 2018 katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Longido.

Wakitoa kifuta Machozi/Jasho  leo Mei 13, 2019 wawakilishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Mkoani Arusha kutoka Kikosi Dhidi ya Ujangili (KDU) Arusha, ndugu Martina Kalunde (Afisa Wanyamapori) na John Msangi (Mhasibu) mbele ya Afisa Wanyamapori Wilaya ya Longido ndugu Lomayani Saiguran Lukumay kwa wakazi 13 waliomba kuwepo na uthibitisho kutoka kwa watendaji wa Vijiji kuwa wahusika waliyofika mbele yao kwa ajili ya malipo ndio wahusika halali wa matukio hayo ya kujeruhiwa/kuuawa na wanyamapori hatari/wakali.

Martina Kalunde (Afisa Wanyamapori kutoka TAWA) amefafanua kuwa wakazi waliopewa kifuta Machozi/Jasho ni wale waliotambuliwa na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W) na kujaziwa fomu ya Kifuta Machozi/jasho na kutumwa kwa Mkurugenzi Idara ya Wanyamapori Dodoma kuomba malipo kwa wahanga. Baada ya fomu hizo kufika Dodoma Wizara ilimwagiza Mkururgenzi Idara ya Wanyamapori kufanya uhakiki wa madai hayo kwa kufika kwenye Wilaya husika. Kwa Wilaya yetu Uhakiki wa Wizara ilifanyika mwezi wa pili 2019 na kubaini wananchi 11 waliojeruhiwa majeraha ya muda na 02 kuuawa na wanyamapori hatari/wakali. Matukio haya yaliwahusisha wanyamapori aina ya Tembo, Nyati, Simba na Fisi.

Afisa huyo aliendelea kwa kutoa ufafanuzi juu ya malipo hayo na kusema kwamba, kwa mujibu wa Kanuni ya Kifuta Machozi/Jasho ya mwaka 2011, mtu akiuawa na mnyamapori hatari atalipwa kiasi cha shilingi za Kitanzania 1,000,000 kama Kifuta Machozi, 500,000 kama amepata ulemavu wa kudumu na 200,000 kama ni mjeraha ya kupona baada ya muda. Aidha aliorodhesha kwa kuwataja aina wanyamapori waliotajwa kisheria kwa Malipo ya Kifuta Machozi/Jasho na kusema kuwa ni Simba, Nyati, Fisi, Kiboko, Faru, Tembo na Mamba.

Kwa upande wake Afisa Wanyamapori Wilaya ya Longido Lomayani Saiguran Lukumay amebainisha kuwa  kifuta Machozi/Jasho hiki kwa wahanga wa wanyamapori Hatari/wakali ni ishara tosha kuwa serikali iko pamoja na wananchi wake kwa kujali haki na thamani yao.  Aidha aliishukuru serikali kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji (W)  kwa malipo hayo kwa wananchi waliojeruhiwa/kuuawa na wanyamapori huku akisema kwamba malipo hayo yatasaidia kuendeleza uvumilivu wa wananchi kuishi na wanyamapori katika maeneo yao kwa amani.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.