• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

ZIARA YA MBUNGE WA WAFANYA KAZI WILAYANI LONGIDO .

Posted on: November 24th, 2023


"HODI LONGIDO NIMEKUJA  KUWAONA, NIMEFURAHI KUWAONA" Ni maneno yake Mheshimiwa, Daktari Alice Kaijage, Mbunge wa wafanya kazi alipofanya ziara yake na kukutana na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido katika ukumbi wa J. K. Nyerere leo tarehe 24 /11 /2023. Akizungumza na watumishi Daktari Kaijage amewaasa wafanyakazi wote kufanya kazi kwa bidii na kwa ushirikiano ili kutoa huduma stahiki kwa wananchi na jamii inayo wazunguka,sambamba na hilo Mheshimiwa ameiomba idara ya Utawala na Rasilimali Watu kufanya vikao vya mara kwa mara ili kujua changamoto mbali mbali zinazowakuta watumishi kwenye maeneo yao ya kazi sambamba na stahiki zao kama kupanda kwa madaraja, upandishwaji wa vyeo,kuumia kazini na mambo mengi yanayofanana na hayo. 

Mheshimiwa Mbunge ameipongeza serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wake Daktari Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwatazama watumishi wa idara tofauti tofauti kwa jicho la upekee kwani katika miaka mitatu ya nafasi yake kama Rais watumishi zaidi ya 450,000 wamepanda madaraja, wengine wamelipwa stahiki zao za malimbikizo ya mishahara,posho za madaraka  pia imetoa ajira kwa watumishi wakada mbalimbali za utumishi wa umma.

Nae Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Longido Ndugu Dominic Ruhamvya ameishukuru serikali ya awamu ya sita ndani ya miaka mitatu kwa kuwakumbuka watumishi wa umma kwa kuwapatia stahiki zao pamoja na kutoa ajira kwa Watanzania.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Longido Ndugu Clemence Kenyatta amemshukuru Mheshimiwa Alice kwa kuja kuzungumza na watumishi wa umma wa wilayani hapo, pia amemuomba Mheshimiwa Mbunge kufikisha baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo zikiwemo  zile zinazohusiana na stahiki za watumishi, kutoa mafunzo kazini kwa Watumishi wa Serikali ili kuongezea ujuzi wawapo makazini, pamoja na kurudisha sera ya kuwaendeleza watumishi waliopo kazini.

"Asante sana Mheshimwa Kaijage kwa kuja kuzungumzia na sisi watumishi tuliopo Wilayani hapa tunaahidi kutekeleza yale yote uliyo tuagiza kama mlezi na msemaji wa watumishi bungeni tunaahidi kufanya kazi kwa bidii na kuwasaidia watumishi kupata haki na stahiki zao kwa mujibu wa sheria wanapokuwa kazini na hata wakati wanapostaafu"Alihitimiasha Ndugu Peter Matemba Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Wilaya.

Ziara ya Mheshimiwa Mbunge Kaijage ni ya siku moja Wilayani humo ikiwa na lengo la kufika na kuzungumza na watumishi na wafanya kazi kwenye Halmasahauri zote  Nchini. 


Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kazi iendelee.





Imeandikwa na Happiness E. Nselu 

Kaimu Afisa Mawasiliano Serikalini Wilaya. 

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • IDARA YA AFYA ,USTAWI WA JAMII NA LISHE YAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM