• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu sekondari
      • Miundombinu, Mipango ya Maendeleo ya Vijijini na Mjjini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Utawala na Usimamizi wa Rasimamli Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Huduma za Kisheria
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Utalii
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Utalii
    • Huduma za Mapato
    • Huduma zetu Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati ya Maadili ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Barua pepe za Idara na Vitengo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Kituo cha habari
      • Maktaba ya Picha
      • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
  • Vivutio
    • Mbuga
    • Ziwa

ZOEZI LA UGAWAJI WA VISHKWAMBI PAMOJA NA UJAZAJI WA MKATABA KWA WALIMU LAADHIMISHWA RASMI LONGIDO

Posted on: January 13th, 2023


Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Longido ndugu Stephen A. Ulaya leo tarehe 13 Januari 2023 ameongoza zoezi la ugawaji wa vishkwambi kwa maafisa elimu kata,wakuu wa shule za msingi na Sekondari katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Longido

Aidha akikabidhi vishkwambi hivyo kwa watumishi hao Mgeni rasmi ambaye ni Katibu Tawala Wilaya ya Longido ndugu Khamana Simba amewaasa watumishi kuvitunza vishikwambi hivyo pamoja na kuvitumia kwa namna bora kwani kwa kufanya hivyo vitawasaidia sana katika dhana nzima ya kujifunza na kujifunzia  na kuongeza tija na ufaulu wa wanafunzi kwani kwa kutumia vishkwambi hivi tofauti na kurahisisha mawasiliano kidijatali pia vitawasaidia kupata miongozo mbali mbali ya elimu.

Aidha ndugu Khamana Simba ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wake mama Samia Suluhu Hassan kwa kuona ipo haja ya kurudisha vishkwambi hivyo  mashuleni ikiwa na lengo la kuboresha elimu kwa njia ya mtandao.

Pamoja na zoezi hilo ndugu Khamana Simba ameongoza zoezi la usainishwaji wa mkataba kwa walimu wa shule za msingi, sekondari pamoja na Maafisa Elimu kata, mkataba huo ukiwa na malengo mahususi matatu ikiwemo kuhakikisha wanafunzi hususani wa shule za msingi wanajua vema kusoma, kuhesabu, na kuandika wafikapo darasa la tatu ili upunguza wimbi la watoto wasio jua kusoma kuandika na kuhesabu pia kuongeza ufaulu kwa wanafunzi na kuweka mkazo katika  kujifunza kingereza Kuanzia darasa la tatu na kuendelea, pia kila mwalimu kujiwekea mikakati iliyo thabiti na malengo binafsi ya kupandisha ufaulu yaani daraja A, B, C na kuondokana kabisa na daraja F

Nae Afisa Elimu Msingi mwalimu Deusdedit Bimbalilwa Kwa niaba ya walimu ameishukuru Serikali  kwa kuona sababu ya kuchagua idara ya Elimu kwenye ugawaji wa vishkwambi na ameahidi kuvitunza kama miongozo inavyosema. 

'Ndugu walimu tutumie vishkwambi hivi kwa umakini na kuvitunza "alisema mwalimu Gilbert Sombe Afisa Elimu Sekondari wilaya ya Longido.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA June 13, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA UMMA April 12, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA May 15, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA June 25, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • KAMATI ZA MTAKUWWA ZAIMARISHWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA NAMANGA

    August 22, 2025
  • View All

Video

MKUU WA WILAYA YA LONGIDO AUNGANA NA RC KIHONGOSI KWENYE JOGGING YA TANZANIA SAMIA CONNECT
More Videos

Kurasa za Karibu

  • ESS-Watumishi Portal
  • Staff Email

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved.